Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

GANDA LA NDIZI sehemu ya kwanza

GANDA LA NDIZI
SEHEMU YA KWANZA
MTUNZI @hanscharlz @storynzuri
Whtsap +255652486818 Tsh 5000#
.
Ilikuwa siku ya Jumatatu kama ilivyokuwa ikizoeleka kwa binti RECHO kudamka asubui na mapema na kwenda sokoni basi siku hiyo alichelewa kufika sokoni na kukuta baadhi ya wachuuzi wenzake kuwakuta wakiendelea na kupata vile walivyokuwa wakiviitaji na kwenda kuviuza kwenye masoko yao madogo madogo, binti RECHO alipofika maeneo yale alishangaa sana kuona vitu alivyokuwa akitarajia kuchukua kwa siku hiyo vilikuwa vikienda kuisha basi nae alifanya upesi na kupata kile alichokuwa kafata japokuwa kilikuwa ni kidogo sana lakini hakuwa na budi ilimbidi achukue tu. Alichukua na kuweka kwenye ungo wake na kuzunguka zunguka japo kuona kama anaweza pata mahari pengine kuongezea kile alichokuwa kapata kwa siku hiyo, binti RECHO alizunguka sana mpaka hapo alipohakikisha kuwa kalizika na kile alichokuwa kabeba basi nae alianza safari yake taratibu huku akiimba nyimbo zilizokuwa zikimfanya aweze kufanya kazi kwa bidii na juhudi kali. Alipiga hatua kazaa na kukutana na mteja wake wa kwanza siku zote na ndipo aliposhusha bidhaa zake na kumtolea achague huku akisisitiza “vya le oleo hivyo mteja wangu” sauti ile ilisikika kwa mteja yule nae kuanza kuchagua kile alichokuwa akipenda.
“kweli hizi ndizi ni za le oleo wala si uongo RECHO”
“hahahahaha ndio mteja wangu” alicheka Binti RECHO huku akifurahia kile alichokuwa akifanya mteja wake akichagua huku akimsifia
“leo nachukua hivi tu”
“sawa ngoja nikufungie” alijibu Binti RECHO
Alipomaliza kumfungia binti RECHO alishika kifaa chake na kuendelea na safari lakini kabla ajamaliza kuvuka eneo la mteja yule alisikia sauti ikimpa sifa zake…
“na kesho upite niwe wa kwanza maana hizi ndizi ni tamu kweli….”
Nae binti RECHO kusikia vile aligeuka nyuma na kumtizama kisha kwendelea na safari yake lakini alimshangaza sana mteja wake pale alipkuwa akitembea kwa malingo huku akirusha makalio yake basi mteja yule alibaki akitizama na kushindwa kula kile alichokuwa akiendelea nacho mpaka hapo alipofika mbali binti RECHO……

Aliendelea kuimba nyimbo zake huku akifikilia kuwa siku hiyo atauza sana kwani mzigo wake ulikuwa ni mdogo sana huku pia akiwaza pale wengine wakikosa huduma kwa siku hiyooo…….!
Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment