Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

NAMALA Sehemu ya TANO


.
SEHEMU YA TANO
MTUNZI HANS CHARLZ 
instagram @hanscharlz @storynzuri 
Whatsapp +255652486818(10000 Tsh)
.
.

Na kulipo kucha jogoo wa shamba aliwika huku binti NAMALA alikuwa mtu wa kwanza kufumbia macho yake kwani alikuwa ameshazoea lakini kwa upande wa Bwana TUMBAKU hata sauti ya jogoo yule hakuweza kuisikia kitu hicho kilimpelekea binti NAMALA………
.                                                           
Binti NAMALA aligeuka na kuwa mtu wa ajabu na kubaki akimshangaza bwana tumbaku pale alipo shituka na kutaamaki kwa kile alichokione mbele yake huku akijiuliza ni mkosi gani uliomuangukia….
“NAMALAAAAAAAAAAAAAAAAA!” aliita jina lile huku akibaki amepigwa na butwa! Kumwona binti NAMALA akitililika jasho kali na huku nguvu za kibinadamu zilikuwa zikipotea. Alianza kutetemeka bwana TUMBAKU huku maneno yakimwisha na kubaki mdomo wazi huku akitafuta njia ya kuchomoka mahari pale kwani alishituswa na kile alichokiona.
“hahahahahahahhaha” ni sauti iliokuwa ikisikika pembezoni mwake huku naye bwana TUMBAKU akiifatisha sauti ile ghafura alipokuwa akitupa macho yake pande zote alishangaa kujiona kuwa yuko mahara pasipo fahaa kuwa yeye kwani aliona makaburi yakimzunguka na huku akizidi kumtizama binti NAMALA alivyo kuwa akibadilika na kuonekana na kubaki mfupa tu kwenye mwili wake.
Binti NAMALA naye alianza kutoa sauti za ajabu huku akiwa kifuani mwa bwana TUMBAKU na kumweka roho juu kwani ilifikia mahari Bwana TUMBAKU alipoteza kumbukumbu na kubaki akiwa amefumba macho yake lakini hazikupita dakika alishituka…..! na………… .
.
Na kutazama tena kwenye kifuaa chake na kuona mifupa tu ikiwa imemuegama nae ilimbidi achukue jukumu la kujitoa ufahamu kwani haikuwa kazi nyepesi aliumia ujasili nae kuweza kuisogeza mifupa ile na kiwili wili cha binti NAMALA…….
“Ni mkosi gani huu jamani umenikuta” ni maneno yaliokuwa yakimtoka kimya kmya moyono mwake huku akiwa na lengo moja tu la kutokomea mahara pa kupata msaada..
“HAAAHAHAAHAHA!!!!!!!!!!!!” ni mara ya pili sauti ile ikisikika ikicheka kwa kishindo kikali na kumfanya bwana TUMBAKU kutotaka kujivuta vuta mahara pale na kuweza kuitupa ile mifupa iliokuwa imemuegama kifuani mwake…
“nini hiki tena” alijikuta akitoa sauti bila ya kutojijua kuwa sauti yake ilikuwa ikisikika maeneo yale.
Aliwaza na kufikiia sana ni nini afanye kwa wakati ule huku akiwa ka kwisha ondoa masalia mifupa ya NAMALA iliokuwa kwenye kifua chake, ndipo wazo likamjia akimbilie upande wa kasikazini mwa mkono wake.
Alianza kupiga hatua kuelekea alipokuwa akiwaza ni mahara salama lakini ilisikika sauti nyingine ikizungumza….
“Njia unayokwenda si sahihi chukua njia nyingine” nayo sauti ilikata gafra na kumchanganya bwana TUMBAKU huku akiachilia mbali aliona ni vyema kuifata njia ile licha ya kuwa na uoga mwingi ilimbidi afanye vile kwani hakuwa na uelewa wa mahari pale.
Alichomoka kwa spidi kali huku ikimfanya ageuge nyuma kuangalia usalama na ndipo alipo……..?
.
Alipogeuka na kutazama kivuli kikimfata kwa spidi kali ae alipozidi kuchanganya kasi ilimbidi ajifiche pembezoni mwa barabara ilia one mwisho wa kivuli kile lakini kilipokuwa kikizidi kumfata nacho kilizidi kufifia kiasi cha kwamba mpaka alipomsogelea maeneo yale alipokuwa kajificha kilikuwa kimekwisha potea chote. Bwana TUMBAKU alishangaa sana kuona maajabu yale huku wazo lake tu ni kufika nyumbani kwake…..
Aliwaza sana yale yaliomtokea wakati akitizama huku na kule ni wapi apite ili aweze kutokomea ili aweze kufika nyumbani… ilimchukua mda kidogo huku akifikilia ni njia ipi aweze kupita wakati ule gafra alishituka pale alipo sikia kitu kikimgusa maeneo ya nyuma huku kikimfanya kujua ni kile kivuli kilichokuwa kikkimfata nae ndipo alipo geuka huku akiwa amejaa uoga…..! alishangaa sana kuona nguo yake ikiwa imenasa na kusababisha kuhisi kuwa ni kitu kilikuwa kikimpapasa maeneo ya mgongo wake.
Alijawa na hakili ya haraka pale alipopata njia na kuanza safari yake aliochukua mda mchache na kufika kwenye kijiji chake. Wanakijiji na ndugu zake walishangaa sana kumwona Bwana TUMBAKU akiwa kwenye hali ile ambayo kila mmoja alitafsiri kivyake licha ya ukweli alikuwa akiujua bwana TUMBAKU mwenyewe, nae hakuongea wakati ule na kupitiliza moja kwa moja mpaka mahari anapolala nae kulala moja kwa moja na alipoamka ndipo alipo waita ndugu zake ili kuwa simulia mkasa wote uliomkuta……………..!
“ndiyo hivyo ndugu zangu nisingeweza kurudi leo hii” alizungumza na kujutia kile alichokifanya kwa binti NAMALA na kuwasisitiza vijana wenzake kutoiga kile alichokifanya kuwa ni hatari kwa maisha yao
Basi kila mmoja wao pale alielewa na kubaki wakiyaweka akilini yale aliokuwa akiwaambia bwana TUMBAKU na wote kutawanyika kurudi kuendelea na shughuri zao huku somo wakiwa wamelielewa kile kilichomkuta ndugu yao……………
                                        

MWISHO
Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment