Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

storynzuri UTAMU WA TUNDA sehemu ya ishirini na Tatu


.
.
UTAMU WA TUNDA SEHEMU YA 23
MTUNZI HANSCHARLZ
INSTAGRAM @hanscharlz @storynzuri
Whtsapp +255 652486818 kwa 5000# tu.
.                         
Ilipishia
“hahahahhahaha sawa” alicheka na kumminya sehemu ambayo kijana Hans alipata raha huku akimwambia
“hapo hapo Happy”
.
“mmmmmmh wapi Hans?
“juu kidogo ya kiuno………!”  Hans alijibu huku akivuta ule utamu uliokuwa ukipenyeza kwenye mgongo wake
Happy aliendelea kumpa kitu roho inapendaaaa mpaka hapo alipoona kijana karithika na kumwacha atulie kidogo, Hans aliona kuwa mbimba ya binti Happy ilikuwa ikizidi kushika kasi pale alipokuwa akiipapasaa na kuijulia hali.
“Happy naona mimba inashika kasi vipi wazazi wako wanajua”
“hakuna hata mmoja anayejua Zaidi yangu na wewe”
“kwanini sasa Happy wafanya hivyo huku unaona kuna vitu vinataka kukwamisha ndoto zetu?”
“no Hans mpenzi wangu wewe usijali”
“mambo makubwa haya Happy”
“yah! Najua”
Hans alibaki akimwangalia Happy kwa kile alichokuwa akifanya kwa siri mdogo mdogo Hans alipata usingizi na kusahau kuwa alikuwa anatakiwa kwenda kwenye mizunguko huku Happy akizidi kuchezea mwili wa kijana Hans, Happy alikuwa kwenye kipindi kigumu huku akili yake ikiwaza sana siku ilikuwa umepangwa kufunga Harusi na kijana Clinton kufanya uamuzi ambao alikuwa akiujua mwenyewe kumsaliti kijana Hans au kumuumiza kijana Clinton. Naye yalipopita masaa kazaa huku akiwa getoni mwa kijana Hans huku akiona kuwa mda ukizidi kuyoyoma ilimbidi achomoke kurudi nyumbani, alimwacha kijana Hans huku akikoroma kitandani mwake naye kurudishia mlango na kuelekea nyumbani Happy alifika nyumbani na kuingia ndani lakini aliokuwa akikatiza kolido la sebureni naye alisikia sauti ya mama yake ikimwita.
“Happy Happy Happy………………….!”
“abe mama”
“mbona siku hizi mbili tatu unatoka bila y ahata kuaga”
“Hapana mama nilikuwa hapo kwa rafiki yangu tu”
“rafikiiiiii?”
“ndiyo mama”            
“sawa” naye Happy alijibu na kuelekea chumbani mwake
.
.
Baba Happy alirudi kutoka kwenye mizunguko yake naye alikuja na jipya pale alipomwita mama Happy pamoja na binti yao Happy nae kukaa nao wote ili wazungumze juuu ya kile kilichokuwa kikiendelea juu ya binti yao pamoja na kijana Clinton.
“nimewaita hapa juu ya swala lla kijana Clinton nab inti yetu Happy”
Baba alizungumuza maada ile Happy alishituka na kungoja kile kilchokuwa kikiendelea baba aliendelea tena kuongea, “tuko pamoja mpaka hapo”
“ndiyo mume wangu” mama aliitikia huku Happy akiwa mdomo umejaa mate hawezi kutoa sauti yake,
“jumamosi hii kwa mujibu wa upande wa pili Harusi itafungwa hiyo nikutokana na kijana Clinton kuwa likizo yake ya kukaa hapa bongo itakuwa inafikia tamati hivyo siku hiyo ndiyo imeteuliwa kuwa ya kuwaaga vijana wetu kwenye maisha yao mapya”
“Baba Happy mbona mapema mno”
“weeeeeeee? Mapema…” Baba aliuliza kwa jaziba huku akimtolea mama Happy macho makali, ukweli Baba Happy alitokea kubadilika sana sio kama kipendi cha nyuma mama Happy alikuwa akiwaza hayo.
“ndio mume wangu”
“basi ndiyo tumepanga kutokana na kijana wao kutaka kuondoka nab inti yetu”
“sawa Happy tuko pamoja”  
Happy alishindwa kujibu na kunyanyuka kwenda chumbani mwake na alipofika alilia sana huku akiwaza “nini baba anafanya kwangu” ni maneno aliokuwa akiyatoa kinywani mwake huku akichuluzisha machozi yaliokuwa yakienda moja kwa moja mpaka sakafuni, Baba Happy alibakia na mkewe sebureni huku akiendelea kutasimini juu ya siku ya Harusi ya mtoto wao, ndipo Baba alipo mpa jukumu mkewe kwenda kumfanya mtoto wao ili asije kuwaaibisha siku ya Harusi kwani walimjua fika binti yao alivyokuwa kichaaa asiki wala kuelewa.
Mama alikwenda moja kwa moja mpaka chumbani mwa Happy na kuanza kumtuliza
“mwanangu kubali tu kuolewa na kijana Clinton hana neno mtoto wa watu”
“mama we acha tu ujui ndio maana”
“sawa lakini Baba yako anakutengenezea mazingira usije teseka mbeleni”
“sawa mama” Happy aliitikia vile kumlizisha mama yake naye mama kutoka chumbani mwake.
.
.
Zilipita siku kazaa huku ilikuwa imebakia siku moja kwenda kufanyika Harusi ya Clinton na Happy mtaa mzima ulijua kuwa binti Happy Harusi yake ni siku iliokuwa ikifuata, basi vijiweni usiku Hans katika pita pita yake alikutana na maada hiyo iliokuwa ikizungumziwa Harusi inayo kwenda kufanyika ni ya kimataifa kwani vijana waliokuwa wakizizungumza walikuwa wakitia na chumvi kiasi chake
“heeeee mtoto mmoja hapo kati mzuri kishenzi kesho Harusi yake”
“heeeeee yupi huyo mwanangu” kijana mmoja alidakia
“si yule aliokuwa akiutikisa sana mtaaa wa hapo nyuma”
“mmmmmmmh nani huyooo…?”
“haaaaaaah kumbe yule binti Happy” aliitikia kijana wa pembeni
“yah mwananngu ndio huyo huyo”
Hans aliposikia vile aliendelea kusikiliza na kuwaza kwani siku mbili hizi hakuweza kuonana naye binti Happy na kuwaza kuwa binti Happy kaonesha udhaifu mkubwa,  naye aliingilia kati mjadara ule kujua ni lini na wapi Harusi itafungwa.
“hivi harusi ya huyo dada inafugwa wapi” aliuliza kijana Hans
“kanisa la ushuwani…” alijibu kijana aliyekuwa akijua na mahari gani panapo fanyika harusi ile
Hans alitoka mdogo mdogo mpaka getoni mwake na kujitupa kitandani mwake na kuitafuta picha aliowai kumpatia kipindi cha nyumba binti Happy naye alianza kuitazama huku akifikilia zile za chinichini alizokuwa akimpeleka binti Happy kwenye kilele, aliwaza sana ni wapi atapata kuponea kama sio kwa binti Happy alipitiwa na usingizi mpaka asubui.
Kulikucha siku ya Jumamosi nayo familia ya Baba Happy ilianza maandalizi ya mwanao kwenda kanisani huku mda ulikuwa umepengwa kwa wawili hao kufunga ndoa ulikuwa ukishika kasi pale ilipofika saa sita mchana, kwa upande wa kijana Hans naye alichelewa sana kuamka kwani alikuwa kalewa chapaka chapa naye alipoona masaa yakizidi kushika kasi alichomoka kitandani na kuanza kuzikamata njia za kwelekea kanisani………..
Ilipofika wakati Clinton ndani ya suti pia Happy ndani ya shela huku wakisindikizwa na zigeregere na vifijo mpaka mazabauni mbele ya padre Clinton alimvua shela binti Happy ili wamalizie hatua ya mwisho, padre alianza kubaliki ndoa ile huku ikifata sauti za wawili hao kukubaliana kuwa mwili mmoja katika maisha yao…..
“Clinton pamoja na Happy sogereaneni” ni maneno yaliokuwa yakitoka kwa padre
“ndugu Clinton umekubali kumpokea binti Happy awe mke wako wa kufa na kuzikana….”
“ndiyo nakubali” aliitikia kijana Clinton
“nawe Happy unakubali kuwa na Clinton awe mume wako wa kufa na kuzikana”
Ukimya ulitawala kwa binti Happy huku padre akingoja tamko la binti Happy naye alirudia kwa mara ya pili gafra sauti ilisikika ikitokea nyumaaaaaaa…….?
.
JE NI SAUTI YA NANI ILISIKIKA?


Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment