Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

storynzuri UTAMU WA TUNDA sehemu ya ishirini na nne


.
.
UTAMU WA TUNDA SEHEMU YA 24
MTUNZI HANSCHARLZ
INSTAGRAM @hanscharlz @storynzuri
Whtsapp +255 652486818 kwa 5000# tu.
.                         
Ilipishia
“nawe Happy unakubali kuwa na Clinton awe mume wako wa kufa na kuzikana”
Ukimya ulitawala kwa binti Happy huku padre akingoja tamko la binti Happy naye alirudia kwa mara ya pili gafra sauti ilisikika ikitokea nyumaaaaaaa…….?
.
“Happy unanisalitiiii” ni sauti ya kijana Hans ilikuwa ikisikika huku akisogea eneo la tukio,
Waumini na wote waliokuwa kwenye misa hiyo walipigwa na butwaa pale binti Happy aliposhindwa kuvumilia na kutoongea nae kutoka mbio mbele kwenye madhabau na kumfata kijana Hans, Nae alipomfikia kijana Hans aliwageukia waumini na wageni waalikwa nae bila y ahata woga alizungumza…..!
“huyu ndiye nilie pendezwa naye” aliongea maneno yale machache bint Happy na kumshika mkono kijana Hans kutimuka wote kutoka ndani ya kanisaa.
Wazazi wa pande zote mbili walibaki wakiwa kwenye mshangaoo wa hali ya juuu huku mama Happy alikuwa akilaanai sana huku akimlalamikia mumeweee kwa kile alichokuwa akitaka kifanyike sasa kinawatia aibu…
“mume wangu nilikuambia mtoto  yule alivyoooo…!”
“mke wangu sikujua haya yote”
“sasa unaona hizi sura zetu tunazificha wapi?”
“mke wangu mda huuu si wa kulalamiiana” Baba Happy aliongea maneno yale huku akiinamisha kichwa chake kwa ile aibu iliokuwa ikimsonga kichani mwake, basi nae ilimbidi apite mlango wa nyuma ili kukimbia umati ule.
Kijana Clinton alibaki akishangaaa huku akiwa na padre wakiwa madhabauni wawili hao walikuwa wakishangaana naye padre ndipo alipo muuliza kijana Clinton
“kulikoni mke wako au mlikuja kuongopa mbele ya kanisa”
“hapana padri mpaka sasa sijui kipi kinachoendelea”
“ujui…?”
“ndiyo sijui lolote mwenyezi mungu ananiona”
Watu waliokuwa kwenye misa hiyo kila mmoja alitawanyika na kuiacha familia ya Clinton huku wakitafakali kile kilichotokea huku na kule walimtazama Baba yake Happy wala hawakuweza kumwona kwani alikuwa ameshakwisha pita mlango wa nyuma na kuondoka..!
“aibu hiii mke wangu tunaificha wapi” Baba Clinton alizungumza
“kweli hiii aibu mno watu tumewapotezea mda wao wanatuona si sio wa maana”
“mpaka rafiki yangu kakimbia” aliongea huku akishika kichwa naye kuchukua simu yake iliokuwa mfukoni na kumpigia Baba Happy, simu ilipokelewa naye hakuanza na salamu bali alimwagia madingo baba yake Happy mbele ya umati aliokuwa nao huku nao walikuwa wakimpandisha hasila naye kuikata simu huku akiendelea kulalamika kwa kile kilicho tokea, Basi nao walikuwa wamepoteza hela nyingi kwaajili ya kijana wao kuoa basi iliwabidi warudi nyumbani.
.
.
Happy pamoja na Hans walizidi kutimua mbio huku wakielekea mahara pa utulivu na walipofika mahali hapo walipumzika napo kulikiwa na upepo mzuri tena miti iliokuwa ikidondosha maua mazuri ambayo yaliwafanya kukaaa hapo mpaka makija ya jioni huku wakipiga story za kile kilichotokea kwa binti kutaka kumsaliti kijan Hans .
“Happy kwanini ulitaka kunisaliti” aliuliza kijana Hans
“no Hans wala sikuwa na nia hiyoo”
“inamaana nisinge kuja pale ndio ungekuwa mke halali wa yule kibalaka”
“no Hans sijui tu lakini sikutamani iwe hivyo kwani name nilipokuona tu nilijawa na nguvu za kuweza kuongea chochote”
“mmmmmmh sawa”
Mama Happy pamoja na mumewe walirudi nyumbani huku kila mmoja wao alipita njia yake…
Walianza kuojiana kuhusu mtoto wao alipokimbilia basi kila mmoja wao hakuweza kujua mahali alipo naye mama alikuwa akijua mahali alipokuwa akiishi kijana Hans naye mama alitoka na kwenda kumtafuta binti yao lakini cha kushangaza hata alipofika hakuweza kumkuta mtu kwani geto la kijana Hans lilikuwa limewekewa kufuri zito lilimwacha mama Happy kuwa kwenye mawazo kweli basi alianza kurudi nyumbani huku akiwa mnyonge lakini alipozidi kuiacha geto la kijana Hans alimwona Happy pamoja na kijana Hans wakiwa wanarudi naye aliwasubilia mpaka wafike kwani ndiyo ilikuwa njia ya kufika kwenye geto la kijana Hans.
“Mamaaaaa! Unafata nini huku” Happy alimwona mama naye huku kijana Hans alitaka kukimbia naye Happy alipo mshika mkono wake huku akimzuia, mama alimsogelea mwanae Happy…….
“Happy nini ulichofanya…?”
“Mama toka mwanzo mimi niliwaambia kuwa sijapendezwa naye”
“hata kama mwanangu sio kwa kile ulichokionesha leo”
“mama kila mtu huwa na haki ya msingi kuuseea moyo name ndivyo nilivyo fanya”
“hata twende nyumbani”
“mimi mama siendi nyumbani namuogopa Baba”
“kwa kipi hasa unamuogopa baba yako”
“si kwa tukio zima la leo”
“mweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee! Ebu twende nyumbani”
Mama aliongea huku akimtizama kijana Hans alivyokuwa kavaaa nae Happy pamoja na mama yake waliongozana kuelekea nyumbani, na walipofika walimkuta baba kichwa kikiwa kimejaa asila naye alipo mwona tu Happy alianza kupayuka ovyoo mpaka mtaa wa pili ulisikia kwa zile kelele zilizokuwa zikiendelea.
“Happy nini umefanya………….”
“Baba moyo wangu haukulizika na Clinton…..!”
“ohooooo! Kumbe ndiyo kijana yule anakufundisha jinsi ya kujibu wazazi wako”
Hapana Baba lakini sikuwa tayari kwa kile mlichokuwa mkifanya juu yangu name nilikuwa nikikataa lakini hamkuweza kunisikiliza kwa kile nilichokuwa naitaji Dady”
Baba alichoka na kushusha pumzi huku akilegeza Tai aliokuwa kavaa huku akiona kuwa ikimbana sana, ndipo Mama Happy nae akaja juu huku akimlalamikia mme wake juu ya kile alichokuwa akifanya juu ya mtoto wao Happy na ndipo Baba alipo choka na kumwamulu binti yao Happy kumwita kijana Hans kwao ili aje kuwaona wazazi ili awe mume alali wa binti yao
“Basi sawa namuitaji kijana huyo kesho sawa………”
“kweli Baba…..”
“ndio” Happy aliposikia vile moyo wake ulijawa na furaha kuwa Baba yake mzazi naye kalizika kuwa na Hans basi furaha zake zote alizikimbiza chumbani mwake huku akiuchezea mto huku akizidi kumkumbuka kijana Hans alivyokuwa akipeleka mashambulizi kwenye lango lake, kulikucha asubui sana Happy alichomoka nyumbani kwao na kuelekea kwa kijana Hans nae alipofika getoni mwa kijana Hans alipitiliza na kumkuta yuko na taulo lake basin aye alikaa pembeni yake huku akifurahi kupita kiasi huku akimtizama mara nyingi nyingi kijana Hans huku naye Hans alizidi kujiuliza ni kipi hasa juu ya binti Happy nae alifumbua kinywa chake nakuongea………….
“Vipi Happy kulikoni furaha zote hizi…”
“Ungekuwa moyono ungejua nini na furahia Hans.”
“Mmmmmh nambiye basi na mimi”
Happy alizidi kutoa tabasamu lililozidi kumchanganya kijana Hans na ndipo alipo mtazama huku akishika nyuso yake na kuzungusha mikono yake huku akipa maneno mazuri…..
“baby Baba kakubari na leo kaomba twende nyumbani mimi pamoja na wew”
“heeeeeh kwenu Happy?
“ndiyo baby” Happy aliongea huku akimsisitiza kijana Hans kuwa wazazi  wake walikuwa wakimuuitaji….
“naogopa mpenzi”
“wanipenda kweli” ni maneno yaliokuwa yakimtoka binti Happy huku yakifatana…. Huku yakimuamasisha kijana Hans kujibu huku akijiamini….
“ndiyo nakupenda tena sana Happy”
“basi naomba fatana nami leo mpaka nyumbani”
“okay sawa” Hans alijibu kwa kishingo upande huku akijua kuwa happy alikuwa akimtania….
.
.
Hans ilimbidi ajiandae vizuri naye Happy alikuwa na pesa kiasi alizokuwa kachomoa kwa wazazi wake basi waliingia mtaani kwenda kumtafutia kijana Hans japo nguo nzuri naye aonekane kuwa nazifu pindi atakapo kutana na wazazi wa binti Happy, walifanikiwa kupata mavazi yaliokuwa yakiendana na siku ile basi nao walirudi kwenye geto la kijana Hans na kubadilisha nguo ili waongozane na Happy mpaka kwao ili aonane na wazazi wa binti huyoooooo!. Walitoka na kuanza kupiga hatua kuelekea kwao na Happy huku kijana Hans alikuwa ajiamini kama ni kwelia au alikuwa akiota lakini binti Happy alionekana kuwa na nguvu lape alipokuwa akiongea nae huku akimfanya kuwa na ujasiri wa kuongea na wazazi wake licha yake kuwa muuoga…
“karinu Hans…………………” Happy alimkaribisha kijana Hans mpaka ndani
“asante japo mwenyeji hapa”
“naomba nisubilie hapa dakika chache sawa mpenzi…”
“sawa” Hans alijibu huku akiwa na huoga mwingi kwani alikuwa akimwogopa sana mama yake na Happy
Happy alitoka na kwenda kuwaita wazazi wake waliokuwa chumbani, nao waliposikia kuwa kijana Hans kawasili basi walitoka chumbani na kwenda moja kwa moja mpaka sebureni, na walipofika walimkuta kijana Hans akiwa tofauti na walivyokuwa wamezoea basi muonekano ule uliwafanya wazazi washituke na kumwona kuwa kijana mtanashati….
“karibu kijana”
“asante….” Aliitikia huku akitizama chuni huku akiwa hajiamini
“kwanza hongera sana kijana umeonekana kuwa na ndamu nzuri iliompendeza mtoto wetu basi nasi tumelizia kuwa naye…….
“asante baba” Hans alizidi kutojielewa mpaka wakati huo na ndipo alipoitwa Happy
Basi walipomaliza kumkabizi kijana Hans nao walijumuika kwa pamoja kwa chakula kilichokuwa kimeandaliwa nab inti mzoefu Johari, basi Hans alianza kuzoea huku wakicheka na wazazi wa binti Happy. Katikati ya tafrija ile binti ndipo alipo zihilisha kuwa yuko na mimba ya kijana Hans wazazi wake walishanga japokuwa mama yake alikuwa akijua kila kilichokuwa kikiendelea basin ae Baba hakuwa na lolote la kufanya kwani alijuwa wazi binti yao kaishakuwa nae alipopewa taharifa ile wala hakuweza kuijia juu.
Ulipita mwaka mmoja huku binti Happy pamoja na kijana Hans kupata mtoto mmoja wa kiume huku wazazi wake Happy walisaidia sana huku waliwajengea nyumba nzuri na maisha ya kijana Hans yalibadilika pale baba Happy akimwajili kwenye kampuni yake na kumpa kitendo kijana Hans, naye Hans alizidi kuonesha juhudi kwenye kazi huku akimflaisha bosi wake mpaka alipo pandishwa cheo na kuwa na kitengo kikubwa….., Maisha yake yalikuwa mazuri huku akimfanya Happy ndiye jicho lake……………….. huku akilisamini mnooo

……………………………………….MWISHO…………………………………………………..


Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

2 comments: