Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

NAMALA Sehemu ya kwanza





BINTI NAMALA
SEHEMU YA KWANZA
INTAGRAM @hanscharlz @storynzuri 
Whatsapp +255652486818
.
.

Kilikuwa kipindi cha kiangazi katika kijiji cha SOWETO, ilikuwa ni majira ya jioni bwana TUMBAKU alikuwa akirudi zake nyumbani kwenda kumalizia siku, alikuwa akitokea shambani naye kuipita mahala ili ashushe kiu yake aliokuwa katoka nayo shambani naye alipita mahara na kuanza kufanya yake, alikunywa mpaka kuzikinai na huku akiona mda ukizidi kwenda aliaga lakini vijana wenzake walikuwa bado wakimwitaji kwani alikuwa na vionjo pindi walipokuwa wakipata moja moto moja baridi huku akionekana kuwa mtubwizaji……
“haaaaaa! Unataka kuondoka mapaema yote hiii” ilisikika sauti ya kijana mwenzake ikiongea
“ndio kwani nyumbani kwangu mlango uko wazi”
“hakuna wezi kijijini kwetu bwana twendeleee kidogo”
“nusu saaa tu inanitosha………Mama ngeza nyingine hapa”
Waliendelea kupata dozi ya nusu saa huku bwana TUMBAKU akiwa makini sana kuofia kuzidisha kiwango cha kunywa kwa siku hiyo basin aye alikuwa akinywa kwa speed ya chini huku akiona wenzake wote wako chapaka chapa hoi……….
.
Ilifika wakati aliona ni bora ajinyanyue ili aanze safari kurudi kwake kwani kulikuwa na mwendo kutoka pale, basi aliwachomoka na kubeba chupa moja na kuzunguka nyuma ya nyumba ile na kutokomea polini naye alipoipata barabara alianza kutembea huku akiimba ovyo ovyo barabarani….. sauti ile ilikuwa ikisikika kwa wingi wa ukinya kwani kijiji kilikuwa kimetulia mno huku wanakijiji wote walikuwa kwenye majimba yao wamelala.
Bwana TUMBAKU alijawa na wasiwasi kuhusu mlango wake huku akiwaza huwenda vibaka wameshapisha lokoo kwenye nyumba yake basi alizidi kuwai huku akienda akipiga mafundo mdogo madogo njiani, ilifika mahari aliona potelea pote kwani mda ulikuwa ushakwenda naye ilimbidi aanze kwenda mdogo mdogo……., alifika mahari ndege waliaruka kwa fujo na walimtia wasi wasi sana huku akili zake zilirudi naye kushika siraha yake na kutazama kwa umakini sana pande zote naye kusikia vishindo vijija kwa kasi aliwaza ni nini kile naye alikaza siraha yake mkononi na kujiandaa na mapambano.
Vishindo vile vilimfanya kujirudi kiakili naye ndipo alipojificha kwa pembeni na kukitazama kishindo kile na kuona ni kitu cha kawaida tu alijizarau
Na kuendelea na safari zake, lakini alipokuwa akizidi kupiga hatu aliona kitu kwa mbele yake kilicho mtia wasi wasi lakini aliona ni kama cha mwazo basi alitamba barabarani, lakini kadri alivyo kuwa akikisogelea aliona ni cha utofauti wa hali ya juuu naye ndipo alipoona mtu akiwa juu ya farasi nae akija kwa sipidi iliomuogopesha bwana TUMBAKU na kutaka kujificha lakini alishindwa pale alipomwona msichana ndiye anaye ongoza ile farasi….
Bwana TUMBAKU alishika siraa yake huku akirudi nyuma nyuma akisogea maeneo mazuri, lakini wakati alipokuwa akirudi nyuma alijikwaa kwenye jiwe naye kudondoka chini lakini bwana TUMBAKU alikuwa shupavu naye alinyanyuka haraka na kuangalia usawa wa kukimbia naye alitoka ndukiiiiiii………….. mpaka mahara pasipo na msaada basi binti yule aliyejulikana kwa jina la NAMALA alipoona kile kitendo cha bwana TUMBAKU kukimbia kilimfanya kuwa na wasiwasi “kwanini alikimbia” alijiuliza na mwisho wa yote alimwamulu yule farasi kwa viboko huku akimwongoza njia naye kumfatisha mahara alipokuwa akikimbilia…..
.
.

Bwana TUMBAKU aliishiwa na nguvu za kukimbia huku akibaki ameshika magoti yake na kutazama mahali pa zuri ili ajifiche kwani aliona binti yule kwa kumwangalia alikuwa ni hatari. Licha ya kuwaza vile bwana TUMBAKU alipata mahara pa kujificha naye kuingia vizuri na kutokomea kwenye upenyo uliokuwa ni mkubwa kwake.
Binti NAMALA alizidi kuzifuata nyayo za Bwana TUMBAKU mpaka hapo alipoona hana mwelekeo wa kumwona bwana TUMBAKU naye alibaki akijiuliza yuko wapi lakini kwa uwezo aliokuwa nao binti huyo hakuweza kuishia pale naye alizidi kuzikata mbuga na kuzidi kumfata na kunusa harufu za bwana TUMBAKU. Alifika mahali binti NAMALA aliona nyayo za yule mtu aliye kuwa akikimbia naye si mwingine ni Bwana TUMBAKU zikiishia kwenye kichaka naye kuona vile alijua mahali pale kuna njia ya chini chini ambayo ilikuwa ikitoka upande wapili basi alimgeuza farasi wake na kuelekea mahali palipokuwa na njia ile…… aliwai na ndipo alipokuwa kabaki akimgoja naye aweze kutokeza ili amkamate vizuri bwana TUMBAKU….. licha ya bwana TUMBAKU alikuwa kwenye akipita kwenye vichochoro vile wala alikuwa
Hajui mahali alipokuwa akienda naye ndipo alipoona mwanga na kujua kaishafika upande wa pili aliwai na kufika naye alipo toa kichwa chake alishanga sana kuona… sura ya binti NAMALA ikimwangalia kwa hasira kali na iliompekea kudondoka mwenyewe lakini alijitaidi na kunyanyuka mahali pale na kutaka kurudi tena ndani ya ule uchochoro…..
Bwana TUMBAKU hakuweza kurudi kwani dhoruba alizopata mle ndani zilikuwa sio za kitoto basin ae kuangalia upenyo mwingine na kukimbia. Na ndipo iliposikika sauti ya binti NAMALA ikimwita bwana TUMBAKU….
“wewe kijana simama hapo mara moja nakuambia…………?”
.
Bwana TUMBAKU alishitushwa sana na sauti ya Binti NAMALA ilipokuwa ikisikika huku naye akizidi kupepea kwa mwendo wa feni huku akipishana na upepo na kuacha vumbi nyuma…
NAMALA alimwelekeza farasi wake nae kuanza kumfata kwa kasi iliompelekea Bwana TUMBAKU alipokuwa akimwangalia nyuma binti yule aliona akizidi kumsogelea kwa kasi ya hatari…… ndipo alipokuwa akizidi kugeuka nyuma aliruka hatua mbili na kujikwaa chini na kudondoka chini na ndipo hazikupita hata sekunde nae binti NAMALA alifika eneo la tkio na kumkuta yuko chini na kuanza kumzunguka huku akimchanganya Bwana TUMBAKU mahali alipokuwa kadondokea….
Bwana TUMBAKU hakuwa na ujanja wowote wakati ule naye alisubilia tu kile atakachofanya binti NAMALA huku naye akipumua haraka haraka na mapigo a moyo wake yakimwenda mbio huku akijua ndio mwisho wake basi naye alibaki akitizama kile alichokuwa akifanya binti NAMALA
.
.
Binti NAMALA alicheka kwa kicheko cha zarau huku akimwangalia sana Bwana TUMBAKU…
“hahahahhahahhahaaaaaa kijana msitu huu tunaujua sisi” alicheka na kumalizia na manen ambayo yalimfanya bwana TUMBAKU kujijua kuwa ndio umefika mwisho wake lakini cha kushangaza alimwona Binti NAMALA akiinama na kutoa kitu ambacho kilimfanya kujiuliza kwa mara nyingi nyingi anataka kufanya nini ili aweze kukizuia kwa uwezo wa kuokoa maisha yake naye Binti NAMALA alishika……………..”
.
Naye bwana TUMBAKU alishindwa kuzizuia mbini za binti NAMALA pale alipo msogelea na
Kumweka kwenye mikono yake huku binti huyo alikuwa akicheka pindi alipokuwa akimtizama bwana TUMBAKU huku akinena kwa mdomo wake
“bwana hapa ndio umefika kwa binti katiri kuliko mabinti wote humu porini”
Bwana TUMBAKU alitoa macho na kubaki akimwangalia sana binti NAMALA kwa kile alichokuwa akikiongea naye ndipo alioona ni vyema kutumia njia ya pili…. Kwa kutaka kushika siraha yake, lakini hakuweza kwani binti alikuwa kaishamwona muda mrefu sana huku binti huyo alingoja tu afanye kile kitendo naye amwingilia vizuri.
“unataka nini kwangu binti?” Bwana TUMBAKU aliuliza huku akionesha sura ya unyonge kwa binti aliyeonekana kuwa na majigambo makali..
“hahahhhahahahha”  Binti NAMALA alicheka kicheko kilichomshitua tena Bwana TUMBAKU
“mbona unacheka hivyo kulikoni?”
“basi tu nakuurumia hapa”
“kwa kipi tena binti”
“unavyoonekana tub ado sana uwezo wa kuniponyoka mimi”
“haaaaaaah hilo ndilo limekufurahisha”
Bwana TUMBAKU aliongea naye kutizama kwa pembeni aliona binti kaifazi chupa lenye maji naye ndipo alipoona si budi kumwacha kumwomba japo atulize kiu aliokuwa nayo….
“samaani dada…….”
“bila samahani” aliitika Binti NAMALA huku akionekana kuwa makini sana
“nisaidie japo fundo moja la maji yako”
Ilimchukua takiribani dakika kazaa mpaka alipopata nini afanye naye alionekana mdogo mdogo akigeuza shingo yake ili aweze kumsaidia Bwana TUMBAKU……
“sawa haya hapa”


USIKOSE SEHEMU INAYO FATA HAPA HAPA 

Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment