Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

GANDA LA NDIZI sehemu ya NNE

GANDA LA NDIZI
SEHEMU YA NNE
MTUNZI @hanscharlz @storynzuri
Whtsap +255652486818 Tsh 5000#
.        
Basi binti RECHO alishika chombo chake kwa umakini wa hali ya juu na kuangalia pande zote huku akiona ziko shwali basi ilimbidi achukue maamuzi magumu pale alipochomoka kwa sipidi ya ajabu mpaka kupelekea kijana yule kubaki akipigwa butwaaa Zaidi ya dakika kazaa zilipita huku akimtizama binti RECHO….. alishika kichwa chake na kugeuka ili aendelee na shughuri zake mahali pale basi alimenya ndizi ya kwanza na kula pale pale aliona ni tabu sana na kubaki akimtizama mpaka alipoisia binti RECHO..
RECHO alizidi kupiga hatua zake nyingi mpaka kupelekea kujikwaaa lakini amanusura adondoke lakini kwa uwezo wake na mzoefu wa mazoezi zoezi la kudondoka lilishindwa.
Alisonga mbele lakini wakati akitokomea mara gafra alikutana na binti mmoja aliyekuwa akijulikana kwa jina la VICK. VICK nae alikuwa akielekea kazini majila hayo ya asubui licha ya kupenda sana ndizi za binti RECHO ilimbidi amsimamishe lakini alipokuwa akidiliki kumwita binti RECHO alimwona kuwa mawazo yake hayakuwa mahali pale basi alimgoja na kusimama mbele yake na kumshitua….
“kulikoni ndugu yangu mawazo yanatoka wapi?” aliongea VICK na kumwacha binti RECHO akitizama nyuma nae kumwona kuwa huwenda anakimbizwa basin ae aliona ni heri kutupa macho yake kule alipokuwa akiangalia binti RECHO. Hakufanikiwa kuona kitu licha ya kumwona kijana mmoja akiendelea na mambo yake basi alimshika mkono binti RECHO na kumwambia……………..
“kulikoniiiii leo biashara unauza kweli….”
“ndio dada yangu” alijibu huku akiwa na mashaka mwilini mwake
“sawa mbona unaangalia sana ulikotoka kulikoni”
Hamna chochote!!!! Matunda ni ya leo leo dada yangu” alikata maongezi yale na kuingia kufanya biashara wakati huo….
“hata mimi naona ni vya lee leo ni bei gani leo”
“kama kawaida dada bei haijabadilika ni ile ile” alijibu RECHO
“naomba tunda moja nionje hapa” alipewa nae kula na alipomaliza alilipa pesa na kuendelea na safari………………..

VICK alipiga hatua zake huku akila tunda lake mpaka pale alipolimaliza na kushika kasi kuelekea kazini kwake…. 
Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment