Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

storynzuri UTAMU WA TUNDA sehemu ya ishirini na moja



.
.
UTAMU WA TUNDA SEHEMU YA 21
MTUNZI HANSCHARLZ
INSTAGRAM @hanscharlz @storynzuri
Whtsapp +255 652486818 kwa 5000# tu.
.                         
Ilipishia
.
Mama alikwisha kuongea yale naye kumkaribisha kijana ili aingie chumbani mwa binti Happy naye aliingia na ndipo alipo mtazama Happy kijana yule moyo wake ulikwenda mbio sana….?, na kumsogelea kwa ukalibu binti Happy huku naye Happy alipomwona kijana Yule wala hakuwa na raha yoyote ile ila alitaka kumfurahisha nafsi yake tu.
.
“mambo Happy!”
“poa” aliitika kwa kinyonge binti Happy huku akimtizama kijana yule ambaye hakuwai hata siku moja kumwona licha ya kuwa akisikia tu taharifa zake kipindi yuko masomoni naye,
“naitwa Clinton”
“nafurahi kukujua Clinton” alijibu huku akitizama chini binti Happy
“okay sawa Happy natumaini tutajuana vizuri” Clinton aliongea huku akimwachia tabasamu kali binti Happy naye kutoka chumbani mwa Happy na kurudi tena sebureni alipokuwa kamwacha baba yake pamoja na wazazi wake Happy.
Alifika sebureni na kukaa pembeni ya baba yake na kusonya naye kidogo huku akimsifia kuwa kamchagulia msichana mzuri
“daaaaaah! Dady Happy kweli Happy kweli name nimeridhia kuwa naye binti huyu”
“mmmmmmm! Kweli mwanangu!”
“yah! Dady”
Basi mama Happy pamoja na Baba Happy walikuwa wakimtizama Baba yake Clinton pamoja na mtoto wake wakiwa kwenye hali iliokuwa ikiwalidhisha kwani walipokuwa wakinong’onezana tabasamu kwa mbali kuonesha kuwa Clinton kampenda binti yao licha ya kumwona siku ya kwanza basi wazazi wake Happy walishikana mikono huku baba mtu akiwa kwenye tabasamu kali na mama naye huku akiwa hana furaha yoyote ile kwani alikuwa akijua kuwa binti yake anamimba ya kijana Hans, ndipo Baba yake Clinton alipoona mda wake wa kuwa pale umefika tamati ilimbidi ajiongeze kuaga familia ya binti Happy ili wakajipange vizuri kuja kumchukua binti Happy ili akaishi na mwanae Clinton.
“haaaaa! Mzee mwenzangu mimi mda umenitupa mkono kuna mahali nahitajika tutazidi kupanga na kufanikisha zoezi hili”
“okay sawa mzee mwenzangu name sitakutupa mkono tutalifanikisha”
Walishikana mikono wawili hao na kuondoka kwa baba yake Clinton, Baba Happy alimtoa mzee mwenzake na aliporudi ndani mama Happy alikuwa akimsubilia kwa hamu sana sebureni ili kufunguka kwa kile kilichokuwa kikiendelea nyumba ya pazia kwa binti yake.
“mumewangu mwanao kama unavyo msikia kukubali kwa hili unalo taka kufanya kwa sasa”
“mkewangu acha fikira hizo siku zote nakuambia mimi ni kichwa cha familia Happy atakubali tu?
“mmmmmm!” ulisikika mguno wa mama Happy pembeni na kubaki akijisemea mwenyewe juuu ya jambo hilo
.
.
Happy alibaki chumbani akiwaza nini afanye juuu ya kile baba yake anachotaka kumlazimisha kufanya huku moyoni mwake hakukuwa na makubaliano ya kitu hicho, aliwaza sana huku akibadilisha mapozi kitandani mwake na ndipo alipoona njia sahihi ni mama yake naye alitoka chumbani mwake na kuelekea sebureni na kumkuta mama kashika kichwa huku akiwaza sana naye taratibu alijisogeza mpaka pembezoni kidogo kwa mama yake alipokuwa kaka naye kumshika kwa nyuma, mama alishituka sana.
“we Happy kulikoni”
“hamna mama nimekuja tu nakuona uko na mawazo mengi”
“ungejua mwanangu hapa nakufikilia wewe tu”
“mama mimi tena!!!!!! nini hicho”
“kuolewa mwanangu na kijana Clinton baba yako yuko na msimamo wa hali ya juu”
“mama mimi kuolewa naolewa lakini siyo kwa mtu ambaye sijapanga kuolewa naye”
Mama happy alishika kichwa chake aliposikia yale maneno yaliokuwa yakitoka kinywani mwa binti yake na kumfanya kuchanganyikiwa Zaidi, na ndipo mama alipo nyanyuka mahali alipokuwa kaketi na kusimama.
“mwanangu unasemaaaa nini au sijakueewa?”
“mama mimi sitoolewa na mtu ambaye sijapanga kuolewa naye” Happy alijibu huku akiwa na msisitizo
“mwanangu kaa chini na fikiria sana kauli zako hii bahati mwanangu”
“mama mapenzi si pesa……………..!!!!” Happy alimalizia kusema vile na kurudi chumbani mwake kuendelea kuuguza kidonda chake cha kufikilia ni jinsi gani wataweza kufanikisha kumwelewa kijana Hans na siyo Clinton.
Mama alimwangalia mwanae Happy akiondoka huku akiwa na msimamo wake ule ule huku ukimfanya kuchanganyikiwa Zaidi naye kujitupa kwenye sofa lililopo karibu na kupitiwa na usingizi uliochukua takiribani nusu saa, alishituliwa na mumeweee naye kuinuka na kukaa vizuri.
“Happy yuko wapi” Baba Happy aliuliza
“yuko chumbani mwake”
“okay sawa ngoja nikazungumuze nae”
.
.
Baba Happy alizungumza na kuanza kuufuata mlango wa binti yake na alipofika aligonga mlango naye baba kuingia ndani.
“Happy!!!!!!!!!!!!!!!!”
“yes dady” aliitika binti Happy
“umeona mambo yameiva mwanangu usiniaibishe kwa rafiki yangu”
“Babaaaaaaaaaaaaaaa?”
“nini”
“nimekwisha kukueleza hali yote”
“usitake kuniambia kuhusu yule kijana mimi nilimuruhusu akukate kiu yako tu na siyo vinginevyo”
“ukisema hivyo baba unakosea”
“nakosea nini basi sasa mimi ndio baba yako na nimeshapitisha Clinton akuoe”
“Baba hunipi haki yangu kama mtoto wako” Happy alizungumza maneno yale na yalimfanya baba yake kumwacha hoi huku akifikilia ni kweli ila atafanya nini na ni rafiki yake.
Happy alichomoka chumbani na kumwacha baba yake akiwa ajielewi naye kupita sebureni mkuku huku speed ile ilimchanganya sana mama yake nae mama kumwita akini Happy hakuweza kugeuka, baada yam da mfupi Mama Happy alimwona mumewe naye akitoka kwa speed na alipofika sebureni tu
“mke wangu Happy kapita hapa?”
“ndiyo tena kwa speed kali sana kulikoni”
“mtoto kaishakuwa ana akili sasa duuuuuuh!!!!” Baba alijibu huku akimwangalia nje ya geti, naye hakuweza kumwona.
Happy alitokomea mpaka kwa kijana Hans na alipofika getoni mwa kijana Hans aliweza kumkuta akiwa anataka kutoka kwenda kwenye mizunguko yake ya kila siku naye kijana Hans alipo mwona mpenzi wake Happy alisitisha kile alichokuwa akifanya nan a kuingia naye getoni.
“mpenzi wangu!!!!!!” aliita binti Happy
“yes baby”
“vipi ujaenda tu kwenye shughuri zako”
“yah ndio nilikuwa najiandaaa mpenzi”
“Okay vizuri lakini mpenzi?” alisita kuongea alipokwisha kuongea kitu kile
“lakini nini”
“familia yangu mpenzi”
“nilikuambia Happy wazazi wako hawapendi kuniona sasa na ninavyo mwogopa mama yako si atanipeleka segerea mimi”
“usifikilie hivyo Hans”
“nakwambia lakini mimi ni kijana nakupenda Happy mno”
“kweli nami pia Hans” Happy alijibu huku akitabasamu na kuzidi kuchanganyikiwa huku mawazo yake yote akiwaza ndiye mume sahihi atakaye kuja kumuoa na siyo Clinton…….?
.
JE NI NINI KITAENDELEA USIKOSE SEHEMU INAYO FUHATA HAPA HAPA KUNDINI

NIPO WEEK YA TEST CHUO SO NITAKUWA NACHELESHA SANA STORY
Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

1 comments: