Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

storynzuri Sehemu ya Hamsini na sita shemeji ingiza pole pole


.
.
Sehemu ya Hamsini na sita 

Mtunzi INSTAGRAM @hanscharlz @storynzuri 


ilipoishia "ndipo nilipo mkumbusha kuwa mkewe dada amina atakuwa anamuitaji kwani mda ulikuwa umekwisha kwendaaa nae aliingia bafuni na kujimwagia maji lakini alipokuwa akitoka simu iliita nami kuiangalia simu hiyo na kuikuta ni namba ambayo sihifahamu na kumpatia Erinest na nilipo mpatia tu aliiangalia na kuniangalia mimi?"


alipo kutanisha macho na mimi alijawa na hofu nae aliangalia chini kwa hofu hiyooo na kujiuliza huku nikikosa jibu 
"vipi si upokee simu hiyooo maana imeita mda mwingi mno" Nilimuuliza shem Erinest 
"haaaaah kumbe lakini namba ya kawaida tu na nitamtafuta badaee isabela" Erinest alijibu
sikuwa na budi basi ilinibidi nichukulie kawaida tu na ndipo nilipo baki nikimtizama lakini wakati nilipokuwa nikimtizama nae alishusha macho yake na kututizama pembeni huku akiendelea kumalizia kujifuta maji kwani alikuwa katoka bafuni kuoga. Nae alipo maliza kujifuta mwili na kuwa vizuri ndipo alipojawa na kigugumizi cha kuongea na mimi 
"'haaaaah! haaaaaha isabela nilikuwaa nakuomba ruhusa yako niende kwa dada yako amina nae atakuwa akiningoja mno!" aliongea Erinest huku akiwa na aibu mno 
"sawa wala sijakuzuia shem wewe waweza kwenda" 
Nilimjibu huku nikimtizama kwa macho makali basi alipokwisha kusema yale aliokuwa akiomba nae alifungua mlango na kuondoka maeneo ya hotelini huku akiwa kaniacha nikiwa na mawazo. Basi alipoondoka tu nami nilibaki nikiwaza usiku kucha juu ya simu ile aliokuwa kapigiwa Erinest na huku nikikosa matumaini ya kile nilichokuwa nafikilia kuwa ninaweza kuishi nae kwa yale aliokuwa akinifanyia shemeji Erinest  huku nikiwaza ya kuwa huwenda Erinest yuko na msichana mwingine tena.


Huku nikiendelea kufikilia hayoo gafra wazo liliniingia kichwani mwangu huku likiwa na mawazo mazuri "Kwanini nisiende kwa Erick na kumweleza kila kitu japo ataweza nisaidia"
Nilifikilia sana na kufika hatua ya mwisho kwa kile nilichokuwa nikiwaza huku nikimalizia kusema potelea pote ngoja kukuche niende kwake.
Asubui ilipo fika yangu kichwani nilikuwa nimeshayapanga kwani ilikuwa ni kwenda kwa Erick tu na kumueleza moyono huwenda atanielewa kwani nae ni binadamu basi ndipo niliposubiria kidogo kukuche zaidi na kumpigia simu 
"haloooooo!"
"Nambie isabela" alijibu Erick 
"nikuambie nini zaidi ya kukumisi tu vipi uko wapi mda huuu?"
"kweli Isabela niko nyumbani mda huuu vipi kwani" Erick aliuliza kwa hofu 
"Nimeuliza tu lakini nataka kuja kwako" niliongea huku nikijing'ata ng'ata 
"Karibu sana nami utanikuta kwani sina mpango wa kutoka leo nauguza kidonda nazani wafahamu? alijibu Erick 
"sawa nakuja"
Nilikata simu hiyo na ndipo nilipo anza chapu chapu kujiandaaa kuvaa ili niweze kwenda kwake. Na nilipo maliza tu kujiandaaa vizuri na kujichunguza niko sawa basi nilishika pochi yangu huku simu yangu nayo nikiwa nimeishika mkononi mguuu mpaka kwa Erick.
Nilifika na kugonga kengere huku nikitumia kifaaa kilichokuwa ukutani nacho kilipiga kelele ndani hata sikutumia dakika nyingi sana kwani nilibonyeza mara mbili na ndipo geti kufunguliwa.
"karibu dada"
"Asante nimemkuta Erick"
"yaaaah! dada yupo umemkuta wewe pita ndani" aliongea mlinzi


Niliingia mpaka ndani ndipo nae Erick alinikaribisha 
"karibu sana isabela"
"Asante Erick nimeshakaribia"
"Hukupotea kweli wewe" Erick aliuliza na kuanza vituki vyake basi nami nilibaki nikicheka na kumjibu
"hapana Erick nimefika moja kwa moja toka nitokako mpaka hapa"
"ok sawa nipe habari" Eeick aliuliza
"mmmmmh! Erick mbona mapema habari utazipata tu bado nipo hapa tutafurahi pamoja siku nzima wala usiwe na haraka kiasi hichoo sawa Erick"
"ok sawa nimeuliza tu isabela" alijibu erick
Nilijiuliza nimuingie vipi Erick mapaka kwenye lile jambo ambalo nilitaka kumwambia siku hiyooo huku nikibaki sina maneno ya kumwambia huku nae akionekana kuwa na shauku ya kutaka kujua kile nilichokuja kumwambia pindi nilipo mpigia simu kwani alijiongeza tu kuwa kuna jambo flani nataka kumwambia siku hiyoo basi nae alitia mitego midogo midogo huku nami nikionekana kuwa muoga. 
nami nilipozidi kuwa na ukimya na kuniona niko kwenye hali tofauti basi sikutaka kufichua jambo hilo na kuanza kupiga nae stori za kawaida kwanza huku nikiweka mazingira ya kufunguka kwa kile nilichokusudia kumwambia.


"Vipi Erick Afya yako inaendeleaje?" nilimuuliza Erick
"Nzuri japo bado bado kidogo nafanya mazoezi ya kuuweka sawa mwili wangu mzima kutokana na dokta alichoniambia"
"ok vizuri fata kile dokta alicho kuambia ili dozi iweze kuujenga mwili wako urudi kuwa kwenye hali nzuri kama ya zamani na kumbuka kumaliza dozi yote sawaaa"
"okay nitafanya hivyo wala usijali mimi nafata kile chote alicho niambia dokta" alijibu Erick 
Tuliendelea kupiga stori mbili tatu huku nikiwa namgusia kumwambia jambo flani ambalo hata yeye alikuwa akijua lakini akuweza kujua ni nini nataka kumwambia nae alitaka kukijua japo nilikuwa nikionekana kuwa mda ulikuwa bado wa kumwambia huku nikimwona akielekea nami nikimkatishaaa katisha.
Ilifika mahari uvumilivu ulianza kunishinda huku nikiwaza yale ya hotelini na kuto taka kurudi tena lakini nafsi ilikuwa ikinisukuma kumwambia jambo hilo na ndipo nilipo anzaa kufunguka bila kuwa na kufuli.
"Erick huwenda utanifikiria vibaya lakini nafsi inanisukuma kukuambia jambo linalo utesa moyooo"
"jambo lipi tena isabela" aliuliza kwa mshangao mkubwa Erick 
"jambo hilo Erick ni dogo lakini kwa upande wetu sote ni gumu kuliko lakini naogopa pindi nikuambiapoa utanifikilia vibaya mnooo"
"Niambie tu wala sitakufikilia chochote endapo ukiwa muwaziiii isabela kuwa freee wala usiwe na hofu juuu yangu mimi ni mwelewaaa sawa mama!"
Nilifikilia sana mpaka nikaona kuwa na uhuru flani ambao ulinifanya niwaze kidogo jinsi gani ya kuyapanga maneno ambayo nakwenda kumwambia na ndipo nilipo pata ujasiri ambao sikujua ulitoka wapi na kumwambia Erick?"

JE? NI NINI ALIMWAMBIA ERICK USIKOSE SEJEMU INAYOFATA 


STORY WRITER HANS

GROUP WHATSAPP PAYMENT  TSH 5000 only +255 652486818 TIGO PESA 


.....................STAR..BOY..............












Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment