Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

storynzuri sehemu ya hamsini na saba shemeji ingiza pole pole



.
.
sehemu ya hamsini na saba

Mtunzi INSTAGRAM @hanscharlz @storynzuri 

Ilipoishia "Nilifikilia sana mpaka nikaona kuwa na uhuru flani ambao ulinifanya niwaze kidogo jinsi gani ya kuyapanga maneno ambayo nakwenda kumwambia na ndipo nilipo pata ujasiri ambao sikujua ulitoka wapi na kumwambia Erick?"


"wajua Erick mimi mimi mimi nafanya haya yote kwaaajili moyo wangu unataka nini lakini kwa sasa moyo huuu nilio nao sio wangu"
"sio wako wa nani tena?" aliuliza Erick huku akiwa kanitazama kwa jicho la aina yake
Na ndipo niliposhusha tena pumzi yangu iliokuwa imeambatana na woga mwingi na kumwambia tena "hapana Erick ufikiliavyo sivyo hapa nakuzungumzia wewe tu kwani sifanyi chochote kile zaidi zaidi ya kukuwaza wewe tuuu hapa Erick"
"mmmmh kweli uyasemayoooo Isabela?" alizungumza kwa mshangao mkali tena mkubwa huku akinitizama Erick
Alinifanya nitizame chini kwa kuingiwa na hofu ya kuonekana kuwa uwenda kafikiria tofauti na ninavyo zani ni mtu wa namna gani, japokuwa nilisema kwa hisia zangu zilivyokuwa zikiongoza nami kumjibu tena
"ndio Erick wala sio utani hivyo ndivyo naamaanisha kwani hisia zangu ziko kwako na usinielewe tofauti Erick?
Erick alinitizama kwa kwa mda mrefu mno huku akinitizama nami nikitafakari mwenyewe moyoni huku nikijisemea "Erick sijui unawaza nini na utanijubu nini mie?"
Basi nilibaki nikiwa najiuliza sana na mpaka hapo nilipo mwina akinyanyua mdomo wake na kuanza kuongea 
"sawa nashukuru sana Isabela kwani sikutegemea sana kama wewe leo utazungumza hivi na ungegusa mahari ambapo nilikuwa najifiklia sana juuu ya kuanza kutatua fumbo hilo ambalo umekuja kulitatua wewe kwani nami nilikuwa kwenye harakati hiyooo! na nimefurahi kusikia hivyoo na shukuru sana na pia naomba tena nirudie tena Nashukuru sana Isabela nafikiria kuwa yametimia yale niyaotayooo usiku na mchana."


Alipo kwisha kusema hayo nae akionekana kuwa mwingi wa furaha kwa nafsi yake huku nami nikiwa na amani wakai huo kwani nami nilikuwa nikiofia sana kujibiwa tofauti na nilivyo kuwa nataka lakini yote yalienda vizuri tu wakati alipo nikubalia ombi langu na kuufanya moyo wangu kufurahi hapo hapo na wakati huo huo. 
Ndipo aliponyanyuka mahari alipokuwa na kunifata mimi huku nikiwaza mbona anakuja huku akishindwa kuongea na kuonekana kuwa mtu tofauti kwa kitendo alichokuwa akikikusudi basi alipofika karibu yangu nae kunikumbatia huku nikiwa mpole nami nilimshika vizuri huku nikionesha ushirikiano wa hali yan nguvu kiasi. gafra mahari tulipokuwa tumekumbatiana kwa mda huo alex alitoka mahari alipokuwa na kuja mpaka mahari tulipo kuwa sisi na sote tulishituka mno na ndipo nae aliguna kiasi chake na ndipo aliposema "karibui nyote mezani" nae kuondoka wakati huooo.
Nakutuacha tukiwa kwenye mshangao mkubwa kiasi kwani hatukuwa tunategemea kutokea kwa tukio kama hilo kwani sote hatukuwa nalo kichwani kama angelifika wakati gani basi kila mimi na Erick tuliposhitushwa vile basi kila mmoja alirudi mahari pake na kujiweka vizuri na tuiona sibudi bali kuitika wito wa Alex kwenda mezani basi tulijongea mpaka mezani na tulipo karibia tu Erick alichomoka mbio na kuniwai mbele yangu na kuonesa kunijari pale alipovuta kiti kimoja na na kunikaribisha mezani nae kwa mara ya pili huku kwangu nikibaki kuwa na huoga kwa kuwaza ya nyuma alipotukuta Alex nae kukutana nae macho kwa macho huku hakunesha huoga wowote na kuniweka kwenye wakati mgumu japo kuwa nilikuwa bado sijamzoea.



Basi niliketi kwenye kiti ambacho Erick alikuwa amekwisha nikaribisha na kuanza kula na kunywaa kwa pamoja huku tukifurahia chakula hicho na kupiga stori kazaa mezani hapo. Tulikula na kusaza vyakula alivyokuwa kaandaaa kijana Alex huku mimi pamoja na Erick tukimbwagia sifa na hongera nyingi kwa kupika chakula kizuri na kitamu chenye mvuto sijawai ona japokuwa nilianza kufananisha mapishi yake pamoja na shem Erinest huku nikiwapa wote asilimia ambazo ziko sawa na kuamini ya kuwa wanaume wengi wanaweza kupika chakula kizuri licha ya kufananisha mapishi ya Alex na Erinest huku nikiwaona watundu kwenye sekta hiyooo! Yote hayo nilikuwa nikiwaza kwenye kichwa changu wakati nikiwa bado mezani huku tukiendelea kumpa pongezi kwa kile alichokuwa akikistahiri kwa kuonesha ufundi kwenye chakula cha siku hiyooooo!
Tulipo maliza basi nae Alex alianza kufanya usafi huku nasi ilitubidi tumpishe nae afanye usafi vizuri hapo mezani na kurudi sebureni. Na tulipofika sebureni mimi pamoja na Erick tuliendelea na stori za kawaida tu huku tukiyasogeza masaa mbele kwa siku hiyo huku nami nilikuwa nikiendelea kupiga stori na Erick huku nikiwaza ya kumwingia Erick na kunielewa juuu ya kuto rudi tena hotelini ili ni lale kwake na yawe makazi angu mapya basi huku tukiendelea kupiga stori nami nikiumiza akili ya kumwingia na kunielewa vizuri basi nilikuwa nataka kujalibu lakini nafasi nyingine ilikuwa ikinikatazaaa mpaka hapo nilipoona wakati umefika wa kumwambia na kuanza kufunguka.
"sorry Erick!!!!" 
"yes Isabela" alijibu Erick 
"nilikuwa nakuomba kitu kwa siku ya leo sijui waweza nisaidia????" 
"yah! naweza lakini kitu gani hicho isabela???" aliuliza Erick huku kionesha kuwa na mshangao pindi nilipo muomba kitu ambacho hakuwa na ufamu nacho
"ningependa usiku wa leo nilale mahari hapa"
"okay! sawa lakini vipi kuhusu dada yako anajua kuwa una lala huku au umempigia simu?" aliuliza Erick 


Nami kuanza kujing'ata kwa lile swali alilokuwa akaniuliza kwani ukweli nilikuwa naujua mwenyewe japo sikutaka kumshirikisha kwa hilooo kwa wakati huuu nami ndipo nilipo mjibu Erick.
"yaah anajua kwamba leo niko huku na nitamfahamisha kwa SMS kuwa leo niko huku na nitalala huku wala usijali kwa hilo Erick"
"okay sawa kama utafanya hivyooo Isabela kwani nilipenda kuwa dada yako ajue kuwa niko hukuuu sawa"
"sawa"
Alipokwisha kusema na kuonesha kuwa kanikubalia ombi langu wakati huo nami nilimwomba tena japo nijimwagie maji nipunguze joto nililokuwa nalo kwani pindi alipokuwa akiniuliza maswali huku nami nikimjibu jasho kwa mbali lilikuwa likichuluzika kwani alikuwa akiniuliza maswali yenye kujibiwa kwa hakili mnooo. Nae aliomba nimfate anielekeze mpaka bafuni nipate kujimwagia maji alinifikisha nami kuingia na kuoga na nilipo maliza nilirudi sebureni alipokuwa na kuniongoza moja kwa moja mpaka kwenye chumba cha wageni na kuniambia.
"hapa ndipo utakuwa ukilala isabela sawa mama"
"sawa Erick wala usijali nisha karibia" nilimjibu huku nikimkonyeza kwa jicho la huba nae kuinamisha kichwa chini
"okay sawa utanikuta sebureni nakungoja okay isabela"
"sawa nikimaliza nakuja"
niliingia chumbani hapo na kuanza kuangalia chumba hicho huku nikizunguka kila kona ya chumba hicho. Nilijitupia kitandani na kujisifia kwa nafsi yangu kwa kuweza mumshawishi Erick na kunielewa.


Nilipo maliza ilinibidi nimfate Erick mahari alipo (sebureni) na nilipo fika tu nae kumkuta yuko tofauti na vile nilivyo mwacha na kuniomba nitoke nae tuzunguke mitaani kusafisha macho wasawahili tusemavyooo. Alitoka nje na kuchukua gari nami kupanda na kuondoka huku tukimwacha Alex nyumbani pekeyake basi tuliendelea huku nikiwaza safari hiyo ilikuwa ya kuelekea wapi lakini sikutaka kujiuliza sana na kuumiza kichwa changu kwani nilitokea kumwamini sana Erick wala sikuzani atanifanyia kitu kibaya basi tulipita mitaa mingi mpaka kutokea mjini na ndipo alipofika mahari akakunja kona na kwenda kwenye hoteli ya kifahari alipaki gari na kuniambia tushuke nami nilishuka.
"tumefika isabela"
"okay hapa wapi Erick maana sijawai fika hata siku moja?"
"hooooooh hapa nisehemu moja tulivu sana nimeona leo uko kwangu na umeomba kulala kwetu imenibidi tuje furahi kidogo na turudi nyumbani" aliongeaErick 
"okay sawa naona hata mimi pako kmya sana"
"hahahahahha njee kmya lakini ndani pamechangamka Isabela utajionea mwenyewe!!!!"
"sawa kumbe kuko hivyooo"
  Tulianza kupiga hatua kuwelekea kwenye mlango mkuuu na tulipofika Erick alibonyeza lifti na ilipofunguka tuliingia na kuelekea juuuu gorofa ya 20 na tulipofika na mlango ulipofunguka tuuuu nilibaki nikishangaaa kweliii mpaka Erick kunivuta mkono na kuniambia 
"Tuelekeee huku Isabela tukakae pembeni"
basi aliniongoza kwani mimi nilikuwa mgeni wa vitu hivyo na tulifika pembeni mahari alipokuwa amepachagua na kukaaa nae na muhudumu kufika mara mojaaa nasi kuagiza vinywaji huku vikionekana kuwa vinywaji vingi ni vile ambavyo vina vilevi huku mimi nilikuwa situmiii na kuomba maji tuuuu lakini kwa Erick aliagiza kinywaji hicho hata jina sikumbukiii basi muhudumu alileta kile tulicho agiza na kuanza kufurahia siku hiyoooo lakini wakati nikiendelea kupata moja baridi moja moto. nilijawa na hudhura kidogo na kuomba niende TOILET basi nilinyanyuka na kwenda na kufaikiwa kufanya nilichokuwa nimekusudia na kurudi lakini wakati nikirudi nilipishana na mtu ambaye nilimkisia kuwa namfahamu?

JE ISABELA ATAMJUA VIZURI MTU HUYO NA ALIKUWA NI NANI USIKOSE HAPA HAPA SEHEMU INAYOFATA

WHTSAP GROUP NI TSH 5000 NUMBER +255 652486818 


..........................STARBOY..................










Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment