Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

GANDA LA NDIZI sehemu ya Kumi na moja

GANDA LA NDIZI
SEHEMU YA KUMI MOJA
MTUNZI @hanscharlz @storynzuri
Whtsap +255652486818 Tsh 5000#
.
Vita ile lilichukua taswira mbaya kwa upande wa mji ule kwani haikuwai tokea huku kila mmoja wao akibaki akijiuliza maswali pia kukosa majibu….
Binti RECHO alikuwa akiendelea kuuza matunda yake licha ya kutojua kilichokuwa kikiendelea mtaa wa pili hakuwa na habari kwani alikuwa akielekea kumaliza biashara yake basi alikuwa na mteja wake wa mwisho kwa siku hiyoo huku akimpa huduma huku mazungumzo yakiendelea…
“mmmh ndizi za leo ni tamu umezipata wapi? Mteja aliuliza huku akizidi kula ndizi moja baada ya nyingine
“mmmmh mbana kwa sikuzote napotolea kwani kunautofauti” alijibu RECHO
“yah tena mkubwa sana kwani za leo zinamvuto wa hali ya juu mpaka natamani nisinyanyuke hapa” mteja aliendela kusemezana nab inti RECHO
“sawa nashukuru sana kwa kusifia kile nitoacho” RECHO alijibu na kumwangalia kwa jicho la huba mteja yule….
Mteja yule alishangaa sana kuona jicho la chini chini likitoka kwa binti RECHO nae kuinama chini na kula tunda lake haraka haraka na kusema…
“yaonekana na wewe mtamu kama matunda yako” ni swali la kizushi aliuliza mteja yule..
“mmmmh wala kawaida tum bona” alijibu na kuinama kutupa maganda aliokuwa akitumia mteja yule… basi wakati akiinama kijana yule alibaki macho akiyapepesa huku hakuamini kwa kile alichokiona wakati ule na kuona ni vyema akate mshipa wa uoga na kufunguka…
“mrembo ningependa usiku wa leo nikawa nawe” alimaliza kusema vile alimkonyeza binti RECHO
Hawakumaliza maongezi yao mara walisikia vishindo vya watu wakikimbia huku na kule walishituka kuona umati wa watu wengi ukiwatafa mahari walipo tena wakipiga mayowe huku ikionekana kunya yao kuna kitu kikiwafukuza, RECHO pamoja na kijana yule walishangaa sana nao watu wale walipita katikati yao huku wakiwaalibia mambo yao huku wakimdondosha binti RECHO na chombo kile wakakitupa, RECHO alibaki akishika kichwa chake huku akiona matunda yake yakikanyagwa vibaya vibaya machoni mwake. Hakuwa na budi ilimbidi akae pembeni na walipokwisha nae alirudi nyumbani huku mawazo yake yakiwa kwenye matunda yale kwani ndio uliokuwa mtaji wake…..
…………………………..MWISHO…………….

#Mrstory #storyempire cc @storynzuridaily @storynzurination
Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

1 comments: