Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

KIGODORO Sehemu ya Kwanza



MTUNZI : HANS CHARLES
Instagram @hanscharlz @storynzuri 
SEHEMU YA KWANZA
KULIPO KUCHA KATIKA KIJIJI CHA KISHONKIZO
Ilikuwa Jumapili asubui kumekucha kijiji cha KISHONKIZO jua lilichomoza kwa mbali huku likiashilia ni siku nzuri basi, wanakijiji wa kijiji hicho wali damka asubui na mapema, waliendelea na shuhuru za hapa na pale licha ya kijana aliye zoeleka kwa uchapakazi mzuri kijiji hapo nae alijulikana kama KAPILO, ni kijana mchapakazi sana na alipendwa na kijiji kizima kwa juhudi zake za uchapakazi na kukijenga kijiji hicho, Nae siku hiyo alikuwa akitoka nyumbani kabeba ndoo ya maji kwenda kwenye mto kuchota maji, ambayo alipanga kufanya shuguri zake siku hiyooo.
Alifika kisimani na kuwakuta wadada wapatao watatu huku wakipiga stori juuu ya siku hiyo ilionekana kuwa na sherehe, japokuwa kijana KAPILO hakujua kilichokuwa kikizungumziwa mahali hapo na wadada hao nae alifanya yake na kuchota maji na alipo maliza kuchota maji nafsi yake ilisita nae alitaka kujua kile kilichokuwa kikiendelea siku hiyo japo yeye alikuwa nyuma kidogo kwani hakujua chochote, ndipo alipo wasalimiwa wadada wale.
“Habari zenu wadada wazuri muuuuh wazima wa afya”
“Wazima hofu kwako kijana mchapakazi” walijibu wote kwa pamoja huku wakionekana kumjua vizuri KAPILO
“Samahani sana, wakati nachota maji niwasikia mkizungumzia siku ya leo mwaweza nijuza name kuelewa” kijana aliomba kujuzwa na wadada wale huku mmoja akinyanyua mdomo wake na kusema “mmmmmh wewe kijana hujui kuwa leo kuna KIGODORO mtaaa wa MAPUNGE” aliongea na kubaki akimtizama kijana KAPILO huku akimvutia kwa jicho zuri nae bibti huyo alimkonyeza kijana KAPILO, huku nae kijana hakuweza kuendelea huku akibaki mdomo wazi
“Asanteni na shukuru sana kunijuza kwani name sikuwa najua chochote kile”
Nae kijana KAPILO akipo kwisha kuwaaga alichukua ndooo yake na kuanza safari ya kurudi nyumbani lakini cha kushangaza kila alipokuwa akipita aliona kijiji kiko bize na kila mmoja wao akiendelea na shughuri zake, na alipo zidi kukatisha alianza kuona yale aliyokuwa akiambiwa na madada wale aliokutana nae kisimani, alipozidi kusogea alizidi kusikia mdundo wa ngoma ambayo ilikuwa ikipigwa kwa staili yake huku ikiwa na ustadi wa hali ya juu, nae kwa mbali aliona vijana wakikimia sehemu farani huku nae akielekea huko huko.                       
.
.
Alivyokuwa akizidi kusogea mara alimwona kijana mdogo nae kumsimamisha ili amuulize kilichokuwa mbele huku akiona vikundi vya watu vikizidi kumiminika mahari paliko kuwa panasikika ndoma nzuri,
“Mbona wakimbia hivyo kuna nini huko” alimuuliza kijana huyo
“Kuna ngoma” kijana huyo aliongea hivyo na kutimuka huku aliona kuwa anacheleshwa na KAPILO
Ndipo nae KAPILO alipo ona nae ni bora kuelekea asije kupitwa kwa kile akiskiacho, alizidi kupiga hatua ndefu ili hali nae afike mapema kwani ngoma zile zilivyokuwa akizidi kupiga hatua zake zilizidi mdundo huku sauti ya ngoma ile ilizidi kumchanganya akili kwani hakuwai kusikia au kucheza alikuwa akisikia tu na kusimuliwa.
Basi alichanganya miguuu yake haraka kuwai eneo la tukio lile na alipo karibia huku akiacha hatua chache tu aliona kikundi cha mabinti warembo wakitia hamsha hamsha eneo lote lile, huku nae akizidi kusogea na kuipita njia ya kurudi kwao, nae kijana KAPILO alifika huku akibaki akishangaaa watu wakizidi kumiminika mahali pale nae alijichanganya pasipo kujua anaelekea wapi,
.
.
Kikundi kile kilichokuwa kimesheeni mabinti na vijana waliokuwa wakiuufanya mdundo usikike vizuri walianza kuama mahali pale huku wakielekea mahala husika, nao wote waliongozana huku wakimfanya kijana KAPILO kuungana nao kwani nae alivutiwa nao kwani walikuwa wakibilinga bilinga makalio yao huku wakimwacha hoi bintabani kijana KAPILO nae akawa “karatasi kifata upepo”, basi waliongozana kwa msafara huku wakiimba nyimbo za vijiweni mchanganyiko huku wakitia madoido kwenye sauti na mipazo ya sauti waliokuwa wakitooooa!!!!!!.

KAPILO alikwa kabeba ndooo yake huku nae akiufata msafara ule unako elekea, huku walipokuwa walipita walizidi kuwasomba vijana na watoto waliokuwa wakipenda “VIGODORO” kwani kikundi hicho kilikuwa kikifahamika mno hapo kijijini kwa siku ya jumapili kufanya tamasha mahali popote pale licha ya wazeee kuzuia walishindwa mpaka wakaona njia nyingine ni kuwaomba mizimu ya kijiji hicho kazi nao wazee wa kijiji hicho walipo sikia kuwa siku hiyo kuna “KIGODORO” walitisha kikao cha dharula, 

NINI KITAENDELEA USIKOSE SEHEMU INAYO FATA?
Share on Google Plus

About storynzuri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment